Satoti_chuwa
Afya yako ni mtaji wako
12/03/2026
Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) limewajulisha Waislamu na wananchi wote kwa ujumla kuwa Sikukuu ya Eid El-Fitri itakuwa Machi 20, au 21, 2026 kutegemea mwandamo wa mwezi na kueleza kuwa sherehe za Eid El-Fitri kitaifa kwa mwaka huu zitafanyika Mkoa wa Dar es Salaam.
Taarifa ya leo Machi 12, 2026 iliyotolewa na BAKWATA imebainisha kuwa Swala ya Eid itaswaliwa katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI BAKWATA Makao Makuu Kinondoni kuanzia saa 1.30 asubuhi na kufuatiwa na Baraza la Eid litakalofanyika katika Ukumbi wa Julius Nyerere Convention Centre kuanzia saa 09.00 mchana Inshallah.
Taarifa hiyo imeongeza kuwa Mgeni Rasmi katika Baraza la Eid atakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Kwa niaba ya Baraza Kuu la Waislamu wa Tanzania Mh. M***i na Sheikh Mkuu wa Tanzania Dr. Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally Mbwana amewatakia Waislamu wote Swaumu njema katika kumi la mwisho la mwezi Mtukufu wa Ramadhani na maandalizi mema ya Sikukuu ya Eid El-Fitri huku akiwaomba kuhudhuria kwenye Ukumbi kwa wingi na kwa wakati.
10/10/2024
Kampuni ya ukopeshaji mikopo ya OYA MICROCREDIT imesema imehuzunishwa sana na taarifa mbalimbali zinazohusu tukio la kusikitisha lililosababisha kifo cha Mfanyabiashara na Mkazi wa Mbagala Mlandizi, Kibaha Mkoani Pwani, Juma Mfaume (40) wakati Wafanyakazi wake walipokwenda kudai mkopo nyumbani kwake.
Taarifa rasmi ya Kampuni hiyo kwa Vyombo vya Habari imesema Kampuni hiyo inatoa pole zake za dhati kwa Familia ya Mfaume na kwa Jamii nzima katika hiki kipindi kigumu na kwamba inapenda kuweka wazi kwa Watanzania na Jamii kwa ujumla kuwa haijawahi kuidhinisha wala kutoa mafunzo kwa Wafanyakazi wake kutumia aina yoyote ya nguvu katika urejeshaji wa madeni
“Taratibu zetu ni za kisheria na zinazingatia maadili na tukio hili halioneshi maadili au taratibu zetu za kawaida za uendeshaji, OYA inashirikiana kikamilifu na Mamlaka katika uchunguzi wao na tutaendelea kuheshimu sheria na kudumisha uwazi katika mchakato huu mzima, taratibu zetu za urejeshaji wa madeni zinalenga kuwa za heshima na kufuata sheria na tunachukua hatua za haraka kupitia upya na kuimarisha michakato yetu ya ndani ili kuhakikisha kuwa tukio k**a hili halitokei tena” - OYA.
“Tunaendelea kujitolea kwa dhamira yetu ya kusaidia na kuwawezesha Watu wenye kipato cha chini, na tutaendelea kufanya kazi ili kudumisha imani ya Wateja wetu na jamii tunazozihudumia” - OYA.
Polisi Mkoa wa Pwani wamethibitisha kuwashikilia Wafanyakazi wanne wa Kampuni hiyo kwa tuhuma za mauaji ya Juma Said Mfaume (40) ikidaiwa kuwa walifika nyumbani kwake kwa lengo la kudai fedha za marejesho ya mkopo wa Mkewe ambapo baada ya Juma kuwaeleza kuwa Mkewe hayupo, walilazimisha kuingia ndani kwa nguvu ili wachukue vitu k**a dhamana huku wakimshambulia sehemu mbalimbali za mwili wake kwa kutumia fimbo kitendo kilichosababisha Juma kuanguka na kupoteza fahamu na baadaye kufariki.
20/08/2024
Click here to claim your Sponsored Listing.
Category
Contact the business
Telephone
Website
Address
TABATA KIMANGA
Dar Es Salaam